Saturday 13 June 2015

MAYWEATHER AWAPIKU PACQUIAO NA RONALDO







Floyd Mayweather
Floyd Mayweather
Bondia Floyd Mayweather amekuwa mwanamichezo anayelipwa zaidi duniani miezi 12 iliyopita, kwa mujibu wa jarida la biashara la Forbes. Orodha ya mwaka huu ya matajiri ilionyesha kuwa Mayweather, alikuwa kinara, akijiingizia dola milioni 300.
Mayweather alimpiga mpinzani wake mkubwa kwa alama Mei 2, 2015 jijini Las Vegas


Mayweather alimpiga mpinzani wake mkubwa kwa alama Mei 2, 2015 jijini Las Vegas
Pesa nyingi zimetokana na pambano lake kubwa na Manny Pacquaio, ambaye malipo ya dola milioni 160 yalimfanya awe wa pili. Mshambuliaji wa Real Madrid alikuwa wa tatu kwa kuwa na dola milioni 79.6.

0 comments:

Post a Comment